kama ni mapenzi
–
ya kuniudhi kila saa, ya kunifanya mi kulia
na kama huridhiki
–
na mbona hujasema, ili niweze rekebisha
ilifaa ni mambo shwari
–
nikiamini u kwangu, na kukusifu kwa wazazi
hujali tena hisia zangu
–
sijui tunapokwenda, lakini najua tulipotoka
–
kutoka sitoki nimetekwa nyara
–
kukuwacha siwezi kibarua ngumu
–
nashindwa ni nini ntafanya uridhike
–
nimetekwa ndani, mtandao wa mapenzi
basi nakuomba, uniteke tu bila mateso
–
tazama, nimezama, ndani ya bahari, la penzi lako
–
siwezi, kusonga mbele, kurudi nyuma, sijielewi
–
haya mapenzi ya fujo hayafai
–
kama wanipenda, jaribu kunipa raha
mi nashangaa, watu wakisema
–
eti tunapendana, japo tunazozana
ni vizuri mami, kumba kuwa na siri
–
lakini jaribu, tusuluhishe
bila hivyo, itakuwa mteso
–
wa kuigiza, kwenye mambo bandia
mimi sitaki, mambo ya kujifanya
–
ati tunapendana, tena tunatesana
–
nimejaribu sana kujitoa ndani
–
kila nikipanga napangua mwenyewe
–
natamani sana ungeelewa hivyo
–
mimi mateka, mimi pumbavu (mabusu), wa penzi lako
nieleze ni lini ntakuwa huru
tazama, nimezama...
jaribu baby...mambo, ya kunifanya kumbafu haifai
mambo yo yo yo yo yo...haifai, jaribu baby, tusuluhishe
nimejaribu sana kujitoa ndani...
tazama, nimezama...
haya mapenzi ya fujo hayafai
kama wanipenda, jaribu kunipa raha...(ad libitum)